Posts

Showing posts from July, 2020

ZIJUE FAIDA ZA LIMAO MWILINI

Image
Hizi ni faida saba za maji la limau kwa mwili wako. 1. Husaidia kuongeza maji mwilini Kulingana na wataalamu wa lishe mtu mwenye afya bora anahitaji kunywa maji kati ya lita 2 na 5 kila siku. Maji haya ni pamoja na maji kutoka kwenye vyakula na vinywaji. Maji ndicho kinywaji bora zaidi cha kuhakikisha mwili una maji ya kutosha, lakini badhi ya watu hawapendi maji kawaida. Kuongeza limau husaidia katika kuyafanya maji kuonya vizuri, na huweza kukupa hamu ya kunywa maji mengi zaidi. 2. Ni nzuri kwa vitamini C Ingawa sio moja ya matunda yenye virutubisho vingi vya vitamini C, limao ni bora kwa kuwa kemikali mimea ambayo hupatikana katika tunda hilo husaidia kutibu mafua na mfumo wa upumuaji. Maji ya limao yanatajwa kuwa na takriban miligramu 18.6 za vitamini C. Na vipimo kamili vya kila siku vinavyopendekezwa kwa watu wazima ni kati ya miligramu 65 na 90. 3. Husaidia katika kupunguza uzito wa mwili Utafiti umeonyesha kuwa virutubisho vilivyo katika limau kwa kiasi

JINSI YA KUPIKA CHAPATI ZA MAJI

Image
Vipimo: Unga wa ngano 2 vikombe (nusu kg) Mayai 2 Chumvi Kiasi Kitunguu maji cha kiasi 1 Karoti ya kusaga ( ukihitaji) Mafuta  ya kupkia Nusu kibakuli Maji kiasi Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 1. Tia maji na mayai kwanza katika mashine ya kusagia (blender) kisha 2. Tia unga, chumvi usage ili unga uchanganyike. 3. Mimina katika bakuli, ikiwa unga mzito, ongeza maji kama uwe mwepesi kiasi. 4. Katakata kitunguu maji na karoti uliyosaga vichanganye 5. Weka kikaango kisichoganda (non-stick frying pan) katika moto na uteke unga kwa upawa wa duara uutandaze vizuri katika kikaango. 6. Subiri Chapati ikauke, igeuze upande wa pili huku unaungandamiza na kuizungusha Chapati katika kikaango ili iive. 7. Iinue kidogo Itie kijiko kimoja cha supu, mafuta au samli. 8. Kakaanga hadi Chapati iive iwe rangi ya hudhurungia kama katika picha. 9. Geuza tena Chapati na igandamize gandamize tena kama dakika moja Iive vizuri upande wa pili bila ya kutia tena mafuta kis

NAMNA NZURI YA KUPIKA KEKI KWA KUTUMIA JIKO LA MKAA

MAHITAJI *unga vikombe2 *maziwa kikombe1 *sukari kikombe1 *siagi kikombe1 *baking powder vijiko vidogo 2 *mayai 6 yakienyeji *vanilla matone mawili au limao 1 Zingatia Limao au vanilla hutumika kwaajili ya kupunguza harufu ya mayai kwenye keki.kwahiyo ukikosa vanilla pia waweza kutumia maganda ya limao. Pia andaa jiko lako la mkaa mapema ili lipate joto pamoja na sufuria iliyopakwa siagi ndani ili kuzuia keki kuganda. HATUA *Andaa bakuli lako la udongo na mwiko ambao utatumia kuchanganya mchanganyiko wako *chukua kikombe kimoja cha siagi na utie katika bakuli pamoja na kikombe kimoja cha sukari. *koroga mchanganyiko wa sukari na siagi mpaka pale utakapolainika na chembe chembe za sukari kupotea kabisa *Weka yai moja baada ya jingine huku ukiendelea kuukoroga mchanganyiko wako bila kupumzisha mkono *Weka matone mawili ya vanilla au maganda ya limao huku ukiendelea kuchanganya. *Weka unga vikombe viwili uliochanganywa na baking powder kwenye mchanganyiko wako na endelea kuukor